Friday, December 21, 2012

Mshenga/wedding matchmaker

 
Waliotusaidia na kumbukumbu ya wikiendi iliyopita walikuwa ni Moro Jazz chini ya uongozi wa Mbaraka Mwaruka Mwinshehe. Wimbo ulikuwa Mshenga Namba 1.Leo tunaendelea na Mshenga Namba 2.

Pata picha umejikusanya wataka kuchukua “jiko”.Unamtafuta jamaa ambaye unamuamini na kumkabidhi jukumu la kuwa mshenga. Unampatia fedha azipeleke ukweni ili ukamilishe mchakato. Baada ya hapo, huku ukiwa na imani kwamba kila kitu kinaendelea vizuri, unaanza kupokea barua kutoka ukweni. Unaulizwa “We bwana vipi?”…”kama umeshindwa,sema ili mtu mwingine achukue jiko”. Kichwa kinaanza kukuuma.Umezikwa. Mshenga kakuingiza mjini…

Mbaraka anauliza imekuwaje? Lakini anawaambia “ukweni” msijali,nivumilieni.Nitakuja mwenyewe kumaliza mambo. Burudika…Ijumaa njema
From http://www.bongocelebrity.com/2012/12/13/mshenga-namba-2-moro-jazzzilipendwa/

No comments:

Post a Comment